Friday, March 18, 2011

KUIONA STARS VS JAMHURI YA AFRIKA YA KATI SH. 3,000

Shirikisho la soka Tanzania, limetangaza viingilio vya mechi ya mchujo ya Kombe la Mataifa ya Afrika (CAN) kati ya Taifa Stars na Jamhuri ya Afrika ya Kati itachezwa Machi 26 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alitaja viingilio hivyo kuwa ni kama ifuatavyo; Viti vya Kijani na Bluu sh. 3,000, Viti vya Rangi ya Chungwa (Orange straight and curve) sh. 5,000, VIP C sh. 10,000, VIP B sh.20,000 na VIP A sh. 40,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa Machi 24 mwaka huu saa 2 asubuhi katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Big Bon Msimbazi (Kariakoo), Mgahawa wa Steers (Mtaa wa Samora/Ohio), Kituo cha Mafuta OilCom (Ubungo), Uwanja wa Uhuru, Kituo cha Mafuta Kobil (Buguruni) na Kituo Kidogo cha Polisi Tandika Mwisho.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litatoa asilimia moja ya mapato yatakayopatikana katika mechi hiyo kusaidia waathirika wa maafa ya mabomu ya Gongo la Mboto.

No comments: